Miezi michache iliyopita, vijiji kadhaa katika tabaka Baswagha-Madiwe katika tarafa la Beni jimboni Kivu Kaskazini vilikuwa eneo la mapigano kati ya makundi mawili ya wenyeji yenye silaha, ambayo yalikuwa yakipigania udhibiti wa maeneo haya. Shule na vituo vya afya vimefungwa, na wakaazi wengi walikuwa wamehama eneo hilo. Tangu utilivu mdogo kuonekana katika eneo hilo, kurudi kwa wakazi polepole kunaripotiwa. Tchetche Aliamini, mkuu wa jumuiya ya kiraia ya Baswagha-Lubena, anarejea hapa katika mahojiano haya na Marc Maro FIMBO kuhusu madhara ambayo hali hii imekuwa nayo katika maisha ya kila siku ya watu.
/sites/default/files/2025-04/160425-p-s-invitebenitchetchealiaminisocivbaswaghamadiwe-00-web.mp3