Habari za siku ya tatu asubuhi tarehe 17/01/2024
- Ni hii Leo siku ya tatu ndio imepita miaka makumi sita mitatu tangu Waziri Mkuu wa kwanza wa Kongo Patrice-Emery Lumumba kuuawa huko Élisabethville, jimboni Katanga
- Siku ya pili hii tarehe kumi na sita mwezi wa kwanza mwaka hu tunao inchi ya Kongo inaadhimisha kumbukumbu ya miaka makumi mawili na tatu ya kuuawa kwa Mzee Laurent-Desiré Kabila.
- Kombe la Mataifa ya Afrika Huko inchini Cote d’Ivoire. Inchi ya Kongo yakidemokratia itacheza mechi yake ya kwanza siku ya tatu hii na inchi ya Zambia.
- Msimamizi wa Offisi ya Uchaguzi CENI mjini Kikwit katika jimbo la Kwilu amesimamishwa kazini na viongozi wake.
- Huko Jimboni Ituri, mkusanyiko wa jamii katika eneo la Irumu unahimiza vyama vya kisiasa vinaviopinga matoekeyo ya uchagzu ya wanabunge kwenda ku mahakama ya kikatiba.
- Katika jimbo la Kivu ya Kusini, zaidi ya familia mia mbili zimelala indje kwa zaidi ya wiki mbili katika mtaa wa Shabunda.
- Jimboni Kwilu, tarafa ya mazingira ya mkoa inasema imeona siku hizi kuongezeka kwa maji katika mito kadhaa na vijito vingine katika jimbo hilo.
- Tatizo la maji ya kunywa huko Mbuji-Mayi huko Kasai-Oriental. Vitongoji kadhaa vinavyotumiwa na shirika REGIDESO huko Mbuji Mayi vimekosa maji kwa karibu wiki moja./sites/default/files/2024-01/170124-p-s-kinjournalswahilimatingraceamzati-00_web.mp3








