Habari za siku ya inne jioni
- Ni siku ya inne hii asubuhi ndio magari na hata watu walianza tena kusafari kama kawaida kwenye eneo la mupaka la Kasumbalesa baada ya mzozo uliyotokeya huko .
- Jimboni la Kongo Central, waziri auhusikaye na uchumi anapinga wageni ambao wanachuruza kinyuma na sheria .
- Katika jimbo la Tanganyika, Wizara ihusikaye na Elimu, ilianzisha siku ya tatu huko Kongolo , kampeni ya kusisimua wazizi katika lengo lakuelimisha watoto, wakiwemo wa binti na wanaume .
- Ni kila tarehe sita mwezi wa kumi ndio kunasherekwa siku kuu ulimwenguni wa Ulemavu wa Ubongo .
- Jimboni Nord-Ubangi, wakaadji wanakabiliwa na mafuriko makubwa kutokana na kuu jaa kwa Mto Ubangi.
- Jimboni Kivu ya Kaskazini, mashamba nyingi ya mahindi yanashambuliwa na kuharibiwa na vidudu vidogo kutoka Marekani katika eneo la Rutshuru.
- Mjini Kinshasa, Kazi ya ukarabati ya barabara ya Kimwenza mission imekuwa ikiendelea hadi leo katika mtaa wa Mont Ngafula tangu zaidi ya mwaka mmoja./sites/default/files/2022-10/061022-p-s-kinjournalswahilisoir-00_web_0.mp3