Journal Soir

Habari za siku ya inne jioni tarehe 24/11/2022

  • Serikali ya mkoa wa Kivu Kusini imefukuzwa kazi na kikundi cha wanabunge wa mkoa.
  • Kuacha mapigano tarehe makumi mbili na tano Novemba  saa kumi na mbili jiono, kurudi kwa nafasi za mwanzoni.
  • Huko Goma jimboni Kivu kaskazini, kuna uhamasishaji mkubwa wa vikundi tofauti vya kijamii na watu binafsi walioathiriwa na taabu inayowakumba wakazi wa Rutshuru waliokimbia pa Kanyaruchinya na ambao wanajipanga kuwapa usaidizi
  • Huko Goma, utawala wa adhabu dhidi ya uhalifu na vikwazo juu ya  silaha nchini DRC ulikuwa lengo la mkahawa wa kisiasa ulioandaliwa siku ya ine  hii huko Goma jimboni Kivu kaskazini na sehemu ya masuala ya kisiasa ya MONUSCO. Wajumbe kutoka vyama vya siasa vilivyo mjini walishiriki.
  • Jimboni Ituri, watu kumi na ine, wengi wao wakiwa watoto, wamefariki tangu mwanzoni mwa mwezi Novemba katika kambi ya wakimbizi ya Djaiba katika tarafa la Djugu..
  • Mapambano dhidi ya tabia mbaya katika shule za jimbo la elimu Kwilu 1, ambalo makao yake makuu yako katika mji wa Bandundu, angalau ma inspecta ine wa shule za sekondari na viongozi wa shule watatu wamesimamishwa kazi  na Mkaguzi Mkuu wa Mkoa, IPP,  Jean Pierre Kasonga Mudiay./sites/default/files/2022-11/24112022-p-s-_journalswahilisoir-00_web.mp3