" Watu wengi hujiuliza kama watawachagua wanani ? "

Fichier audio : téléchargez Flash pour écouter.

” watu wengi hujiuliza kama watawachagua wanani?”

* Karine Kakasi,tulisema mara nyingi kama uchaguzi ni mapashwa ya kirahiya inayopashwa kutimizwa na wakongomani wote .Uchaguzi ni kitendo ambacho kila mwanainchi wa ainchi fulani ao mwana memba wa kamati wanajulisha maoni yao wakati wa uchaguzi ao wakati wakuchukua hatua fulani. Uchaguzi huenda kusikika kama pia kama vile maoni yalioyotolewa na kila mtu wakati wa uchaguzi.
Uchaguzi ni pia uchunguzi wa taifa kwa jumla ya rahiya wakongomani kwa kujichagulia viongozi vyao na pia sheria huenda kuongoza jamuhuri ya tatu. Kwanjia aya auchaguzi rahiya inaonyesha imani yake kwa kandidenti huenda kuongoza inchi na vituo vya serkali.
Karine ,kwa kurudilia ulizo lako,tunaweza kujulishaakama kila mkongomani mume ao mke mwenyi kuwa na miaka yenyi kukukbaliwa na sheria, anayo haki ya kushiriki kwa uongozo kisiasa wa inchi, katika shurti zenyi kushimikwa na katiba ta inchi pia na sheria kuhusu uchaguzi.
Kufatana na nukta 9 ya sheria o6kistarioo6 ya tarehe mwezi wa tatu mwaka 2006,kuhusu matayarisho ya uchaguzi wa uraisi wajamuhuri, wa wanabunge la taifa na la majimbo,miji na vijiji,mtu ambaye wakongomani wanaalikwa kumchagua, anapashwa kuwa mkongomani, anapashwa kuwa na umri unao lazimishwa kwa wakati wa mwisho wakupokea makandidenti.Anapshwa pia kuwahuru na haki zake zote za kinainchi na cha kisiasa,na awe na hali ya mchaguzi ao ajitambulishe na kujiandikisha wakati wa kupana kandidenti yake.

rn* Dunia Mukunda,,watu huenda kujiuliza swali lenyi kuelekea hali gani na mwenendo gani kandidenti huenda kuchaguliwa anapashwa kuwa navyo ?

* Karine , ni kwepesi,mtu ambaye wakongomani wanapashwa kumchagua, ni mtu wa kweli mwenyi kupenda inchi yake na rahiya wakongomani. Awe mwenyi elimu ya kutosha na awe mwenyi kukamilika kwa uongozo wa inchi kuhusu siasa ya inchi.Inafaa awe mtu mwenyi kupendelea manufaa ya rahiya kuliko manufaa yake binafsi.Inafaa kusema kama mtu wa aina ile huenda kupatikana kwa njia ya uchaguzi huru , wa kidemokrasia na ule wa wazi.Uwazi wa mpango wa uchaguzi unahakikishwa na komisheni huru ya uchaguzi na kuweko kwa wachunguzi wa taifa na wale wa kimataifa katika vyumba vya uchaguzi na pia washahidi wa wakandidenti, wa vyama vya siasa ao makundi ya siasa.

* Basi ,bwana Dunia Mukunda ,ni nani anaweza kuwa mshahidi ao mchunguzi wakati wa uchaguzi mbali mbali ?

* Karine,inafaa kuelewa kama,huenda kuwa mshahidi ao mchunguzi kila mkongomani ao mgeni mweni kutumwa na kanddenti huru mwenyi kutumwa na chama cha siasa,na shirika la taifa ao lakimataiafa na ambao wanatumwa na Cei kwa kuangalia opresheni za uchaguzi. Mshahidi yule aoa mchunguzi yule mkongomani anachaguliwa kati ya watu walioandikkwa kwa daftari ya wachaguzi.Kutokuweko kwa wachunguzi na washahidi pa mahali ya uchaguzi hakuwezi kuleta matatizo kwa kutokubali kura ya uchaguzi.
Inafaa tukumbushe kama washahidi wanalishwa na watu walio watuma ao kuwataja.
Na kama vile pia wachunguzi hawapo kwa garama ya serkali.,wala ya Cei.Lakini usalama wao unalindwa na serkali.

* Kwa kumaliza, Dunia Mukunda, basi kazi kamilifu ya wachahidi na wachunguzi wakati waoperesheni za uchaguzi ni gani ?

* KARINE, washahidi na wachunguzi wanao kazi kubwa ya kufanya wakati waoperesheni za uchaguzi inchini mwetu. Wanachungua mwenzendo wa uchaguzi, vitu vyenyi haviendeke ambvyo vinaweza kuleta vikwazo kwa mwenendo bora wa uchaguzi.
Kwa mwisho vituo vya upashaji wa habari sawa vile Radio Okapi, vinajulisha kwa wachaguzi ukweli kuhusu mwenendo wa uchaguzi na kusaidia wakaaji kwa kuchungua ukweli wa operesheni za uchaguzi kwa eneo la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo kwa jumla.

Texte de SAMUEL KATSHAKrnOndes CourtesrnTél. : 0998909787rnTraduction en Swahili de DUNIA MUKUNDA