Fichier audio : téléchargez Flash pour écouter.
” Nani anaweza kuwa kandidenti kwa uchaguzi ? ”
* Kila mwanainchi mkongomani mume kama vile mke mwenyi kuwa na umri wa miaka yenyirnkukubaliwa,anayo haki ya kushiriki katika mipango ya uongozo wa siasa ya inchi, kufatanarnna shurti zenyi kupangwa na kura na pia sheria kuhusu uchaguzi.
Kufatana na nukta ya kenda ya sheria sifuru sita/ sifuru sifuru sita, ya tarehe tisa mwaka wa 2006 inayoelekea uchaguzi mbali mbali ya uraisi na ya bunge la taifa,la majimbo, la miji mikuu, na malokaliti, mtu ambaye wakngomani wanapashwa kumchagua anapashwa awe mkongomani, awe na umri wa miaka yenyi kulazimishwa wakati wa mwisho wa kutia makandidenti.Anapashwa pia awe mwenyi huru kuhusu haki zake za kirahiya na zile za kisasa na awe na hali ya mchaguzi ao ajitambulishe na kujiandikisha wakati anapo tia kandidenti yake.
Mkandidenti anajijulisha mwenyewe ikiwa kama ni kandidenti huru,ao anajijulisha juu ya daftari ya chama cha siasa ao kundi la chama cha siasa la eneo la mahali pa uchaguzi aliyojulisha katika maandiko yake.
Lakini inafaa kujua kama ingawaje hali ya uchaguzi,kandidenti anaweza kujitambulisha tuu katika eneo moja la uchaguzi kwa kila daraja ya uchaguzi fulani.
* Namna gani makandidenti kwa kila uchaguzi mbali mbali yanapashwa kujulishwa
* Nukta kumi na munane ya sheria sifuru sita kistari sifuru sifuru ya tarehe kenda mwezi wa tatu mwaka tunao,yenyi kuelekea uchaguzi ya uraisi , wa bunge la taifa, la mjimbo,la miji mikuu na malokaliti,inasema kama kandidenti huru, chama cha siasa ao kundi la kisiasa linajulisha kandidenti kwa Cei.Kujulishwa kwa kandidenti kunapashwa kusindikizwa na kibarua cha kandidenti chenyi kujulisha kama anaitika kuwa kandidenti , kibarua kile kinapashwa kutii shurti za Cei na kusahiliwa binafsi na kandidentirn Awe pia na sura moja ya cheti chake cha mchaguzi, yaani photocopie na kartasi yenyi kujulisha maisha yake, picha inne , cheti cha kuzaliwa. Sura ao alama ya chama chake cha siasa ao cha kundi la kisiasarn Barua ya chama cha siasa yenyi kujulisha kama aliruhusiwa kuwa kandidenti na chama chake na pia awe na kartasia ya kujulisha kama alilipa pesa zenyi kuitajiwa na sanduku ya serkali.
* Wakati gani huenda kujulisha kama kandidenti fulani haikubaliwe.
* Kufatana na maandiko ya nukta 21 ya sheria kuhusu uchaguzi,ukandidenti fulani huenda kukataliwa ikiwa kama hawezi kuchaguliwa,kama hakujulisha maoni yake kwa njia ya barua ao kama alijijulisha katika maeneo mengi ya uchaguzi kwa kura ile ile moja.Inafaa kuhakikisha kama kila ukandidenti haukubaliwe ikiwa kandidenti anajijulisha juu ya madaftari mengi katika eneo moja la uchaguzi ao kama hakulipa pesa zilizolamishwa ao kama yupo juu ya daftari ya wale hawa kulipa pesa.
Kuhusu makandidenti iliyojulishwa na madaftari ya vyama vya siasa ao makundi ya siasa ao pia wakandidenti huru, hao wanatajwa kama hawakubaliwe wakati wanachukua majina ya watu wenyi hawawezi kuchaguliwa, wakati wanao idadi ya kutosha ya wakandidenti kwa idadi ya kadiri iliyopangwa kwa kila eneo la uchaguzi ao wakati wanarudilia jina la kandidenti katika zaidi ya eneo moja la uchaguzi kwa daraja moja. -rnTexte de SAMUEL KATSHAKrnOndes CourtesrnTél. : 00243998909787rnE-mail : [email protected] [email protected]