Journal Soir

Habari za siku ya kwanza jioni tarehe 16/10/2023

  • Mahakama kuu yani Cour de cassation ilianza shughuli zake siku ya kwanza hii kwa mwaka wa elfu mbili makumi mbili  na tatu na mwaka elfu mbili makumi mbili na inne .
  • Jimboni Kivu ya Kaskazini, mji wa Kitshanga, katika eneo la Masisi, uliamshwa na hali ya utulivu siku ya kwanza  hii.
  • Katika jimbo la Mai-Ndombe, hali ya usalama inaanza kuimarika katika eneo la Kwamouth, ambalo lilikumbwa na ukosefu wa usalama unaosababishwa na wanamgambo wa Mobondo, kufuatia mzozo wa jamii za Teke-Yaka kwa zaidi ya mwaka mmoja.
  • Jimboni Ituri, karibu makao mia moja ya  wakimbizi  wa eneo la Nyamusasi yalisombwa na upepo mkali ulioambatana na mvua siku ya sita katika  usulutani wa Bahema Banywagi mtaani Djugu.
  • Katika  mtaa wa Beni jimboni Kivu ya kaskazini, maeneo manne ya wakimbizi yaliyo katika sehemu ya kaskazini ya mji wa Oicha sasa yanapewa  maji ya kunywa. Ni mradi ulioanzishwa na Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu CICR .
  • Katika jimbo la Tshopo, eneo la afya  la Banalia hivi karibuni litakuwa na  maji ya kunywa.
  • Mjini Tshikapa katika jimbo la Kasai, shirika ya kiraia linaonya juu ya wizi wa taa za barabarani zilizowekwa katikati ya mji kati  ya kilalo  la Tshikapa na mtaa wa  Dibumba ya pili./sites/default/files/2023-10/161023-p-s-kinjournalswahilisoir-00_web.mp3