Journal Soir

Habari za siku ya kwanza jioni

 

  • Kumefunguliwa leo siku ya kwanza mjini Kinshasa  mikutano  kuhusu mazingira iitwao PRECOP 27.
  • Mtu yeyote anayetaka kujenga  lazima aulize  mafundi  wanaojulikana katika muundo unaosimamia masuala ya ujenzi  ili kukabiliana na tukio lolote linalotokana na ujenzi usiyofaa .
  • Katika jimbo la  Ituri, watu kumi na wanne  waliuawa na makao makumi matatu  na sita kuunguzwa wakati wa shambulio la waaso wa ADF mwishoni mwa juma huko Kyamata katika usulutani wa  Tchabi kusini mwa mtaa  wa Irumu.
  • Katika jimbo la Kivu ya Kaskazini, raia kumi na mumoja  waliuawa katika shambulio la  waasi wa ADF jana siku ya mungu katika kijiji cha  Beu Manyama, katika sekta ya  Beni Mbau mtaani  Beni.
  • Katika jimbo la Kivu ya Kusini, hali yaendela kuwa  mbovu  tangu  usiku ya siku ya mungu huko Kamanyola, mtaani Walungu, kaskazini mwa eneo la Uvira.
  • Jimboni Kongo Central, zaidi ya wakaadji makumi saba  wa kijiji cha Kimbongo katika sekta ya Boko, mtaa wa  Mbanza Ngungu, hawana tena mahali yakuishi
  • Kasaï ya mashariki:  barabara kuu  mitatu ya mji wa  Mbuji Mayi zitawekewa lami mwezi huu wa kumi kupitiya  mradi  wa Tshilejelu.
  • Katika jimbo la Maniema, karibu mwezi mmoja baada ya kuanzishwa rasmi kwa shughuli ya kuhesabu  wanafunzi wote na  shule za kipekee , operesheni hii inaendela lakini kwa shida fulani kulingana na mkurugenzi jimboni  wa offisi ya uchunguzu SECOPE./sites/default/files/2022-10/031022-p-s-kinjournalswahilisoir-00_web.mp3