Journal Soir

Habari za siku ya pili jioni

  • Waziri wa Mazingira Eve Bazaiba anatangaza kwamba inchi ya Kongo ya Kidemokratisa inakuwa kwa sasa  sawasawa  na Indonesia na Brazili katika mkakati wa kugombea  haki za wakaadji wake .
  • Katika jimbo la Kivu ya Kaskazini, Prince Kihangi,  mwanabunge jimboni  anapendekeza mtaa wa walikale ushurutishwe na mradi wakupewa mkopo wa kaboni
  • Katika jimbo la Kwilu,ma adui  wawili wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya wakuu wa  vijiji vya BUKUSU na FADIAKA, waliokamatwa walipelekwa  siku ya kwanza mjini   Bandundu.
  • Katika jimbo la Kivu ya Kasakazin, Msemaji wa operesheni za kijeshi  Sokola ya kwanza   anatoa wito kwa wakaadji  wa Butembo na eneo zima kuwa waangalifu  ili kupambana  na tishio la kigaidi
  • Katika jimbo la Kivu ya Kusini ,  kuliandaliwa siku ya pili hii  siku bila kazi yoyote katika mtaa na mji wa Uvira na vile vile katika mji wa  Sange.
  • Katika jimbo la Maniema, kiongozi wa kabila ya BANGUBANGU  LULINDI anayeishi mjini kindu anasema kwamba karibu vijiji kumi na kenda  havina tena wakaadji wao
  • Jimboni Tanganyika, meya wa mji wa Kalemie  ametangaza siku ya pili hii kuwepo ugonjwa  wa  kipindupindu katika mji huo.
  • Jimboni Kivu ya Kusini, kilalo cha  muda cha  Cihanda katika eneo la  Nyangezi mtaani Kabare kilizinduliwa  siku ya pili hii./sites/default/files/2022-10/041022-journalswahilisoirh00-00_web_0.mp3