Mwalikwa wetu ni Mratibu wa shirika lisilo la kiserikali kwa maendeleo, elimu ya uraia na utetezi wa haki za binadamu, ADEC-DDH. Katika mahojiano na mwenzetu wa Goma Gabriel Wamenya, muhusika huyu wa masuala ya haki za binadamu, anazungumzia mikakati ya mawasiliano pamoja na matokeo yanayotarajiwa baada ya kuanzishwa wikendi iliyopita kwa kampeni ya uhamasishaji kuhusu katiba ya Azimio la Kimataifa la Haki za binadamu. Kampeni hiyo inafanywa kwa ushirikiano na offisi ya BCNDH ya MONUSCO. Tumsikilize KARPATE TULINABO katika mazungumuzo haya na Gabriel Wamenya./sites/default/files/2023-05/130523_inviteswahili_web.mp3