Journal Soir

Habari za siku ya inne jioni ya tarehe 15/06/2023

  • Ni siku ya inne hii ndio mitihani ya Kitaifa la Uchaguzi, Mwelekeo wa Kielimu na Kitaalamu, TENASOSP ilianza .
  • Huko jimboni Maniema, liwali  wa muda AFANI IDRISSA MANGALA ndiye aliyezindua mitihani hii kutoka shule ya msingi kindu ville mbele ya viongozi kazaa  wa jimbo hili.
  • Katika jimbo la Equateur ,  liwali makamu na liwali wa muda  alialika siku ya inne hii  wanafunzi wenye kufanya mitihani  wa kitaifa wa ya TENASOSP kukimbiza  woga. Lakini kutumika  kwa utulivu. Kwa hivyo, watafaulu katika mitihani hii .
  • Kufuatana na kikao la kumi na nane la wiki ya madini ya Kongo yakidemokrasia, shirika la maendeleo la Marekani linasema liko tayari kusaidia Kongo  kukuza sekta yake ya madini.
  • Maendelo bora ya  uvuvi yakudumu  na ufugaji wa samaki ni shughuli muhimu kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi makumi mawili na mbili,  wanamemba  wa Mkutano wa Mawaziri wa Ushirikiano wa Uvuvi kati ya Nchi za Afrika zinazokuwa kando  na Bahari ya Atlantiki .
  • Katika jimbo la Ituri, zaidi ya visa elfu moja na mia tano vya surua vimeripotiwa katika muda wa miezi minne katika eneo la afya la Nia-nia, yapata  kilomita mia tatu kutoka mji wa Bunia  mtaani Mambasa.
  • Jimboni Kivu ya Kusini,  kampeni  dhidi ya ugonjwa wa kiumbe cha kizazi ilizinduliwa siku ya tatu hii mjini Bukavu  .
  • Ujumbe wa viongozi wa wanamgambo maimai  TWA wakiongozwa na mkuu  wa kijiji Kasebu walikutana siku ya tatu  hii huko Kalemie na waziri jimboni  wa mambo ya ndani wa jimbo la Tanganyika./sites/default/files/2023-06/15062023-p-s-journalswahilisoirgraceamzati-00_web.mp3